Thursday, June 21, 2012

KATIBU MKUU WA UMOJA WA MATAIFA AFUNGUA RASMI MKUTANO WA RIO NCHINI BRAZIL.

Katibu  Mkuu  wa  Umoja  wa  Mataifa Bw. Ban Ki-Moon (Pichani) amefungua  rasmi  mkutano  wa  siku  tatu  wa  maendeleo endelevu  nchini  Brazil huku akionya kuwa muda  hautungoji  kwa  kuweka  sawa  orodha  ndefu  ya matatizo  ya  mazingira.
Nchi wanachama  191  wa  Umoja  wa Mataifa ikiwa  ni  pamoja  na  marais 86  na  viongozi  wa nchi  wanahudhuria  mkutano  huo  wa  Rio.
Mkutano  huo unafanyika miaka  20  baada  ya  mkutano  wa  kwanza  wa dunia, wakati  mataifa  yalipoahidi  kurejesha  nyuma mabadiliko  ya  tabia  nchi,  kuenea  kwa  jangwa  na kutoweka  kwa  baadhi ya aina  za  viumbe. 


No comments:

Post a Comment