Wednesday, May 23, 2012

NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO, SAYANSI NA TEKNOLOJIA JANUARY MAKAMBA ATEMBELEA MAKAO MAKUU YA VODACOM TANZANIA...!!!

 Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia January Makamba akilakiwa na Mkuu wa Mahusiano na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania Joseline Kamuhanda. Makamba alitembelea makao makuu ya Vodacom katika ziara ya kujifunza shughuli za kampuni hiyo. Katikati ni Meneja wa Mahusiano ya Nje wa Vodacom Salum Mwalim.
 Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia January Makamba akizungumza na watendaji wakuu wa kampuni ya Vodacom (hawapo pichani) wakati alipotembelea makao makuu ya kampuni hiyo jijini Dar es salaam katika ziara maalum ya kujifunza shughuli za mawasiliano nchini. Kulia na Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania Rene Meza.
 Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia January Makamba na Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania Rene Meza wakibadilishana uzoefu kabla ya Naibu Waziri kufanya mazungumzo na watendaji wakuu wa Vodacom Tanzania alipofanya ziara ya utambulisho makao makuu ya kampuni hiyo jijini Dar es salaam.


No comments:

Post a Comment