Thursday, May 17, 2012

MCHEZAJI WA KIMATAIFA WA MABINGWA WA LIGI BARA SIMBA SC PATRICK MAFISANGO AMEFARIKI DUNIA.

Mchezaji wa Simba Patrick Mafisango (kulia) enzi za uhai wake akipokea Tsh. 500,000 kutoka kwa Ofisa wa NMB baada ya kuchaguliwa kuwa mchezaji nyota wa mchezo wa Ngao ya Jamii. (Picha na Maktaba).
--------------------------------------------------------------------------------
Aliyekuwa kiungo mahiri mchezaji wa timu ya Simba SC Patrick Mutesa Mafisango raia wa Rwanda mwenye asili ya Kikongo amefariki dunia usiku wa kuamkia leo kutokana na ajali ya gari maeneo ya Tazara jijini Dar es Salaam.
FUNUNU HABARI BLOG, inatoa pole kwa mashabiki wote wa timu ya Simba SC, Watanzania na Wadau wa Michezo kwa Ujumla. Mungu ampumzishe kwa amani, Amen. 


No comments:

Post a Comment